ISIMU JAMII

ISIMJAMII

isimu,isimu vr,hamisi babusa,maudhui ya elimu katika chozi la heri,virtual reality,quivr,inside mt elgin,alex situma,mwamba wa lugha 13th february 2016 [part 2] elimu ya kiswahili,west tv jioni,dennis okari,erick isinta,west tv kenya,gaming,salaam,sakali dalmus,jasper ondimu,virtual,mjadala,dawati la lugha,fasihi andishi,mathias momanyi,mastergamingvr,master gaming vr,soul,mars,tom nyambeka,educational,light academy

Isimujamii  Ni taaluma inayochunguza uhusianouliopo baina ya lugha na jamii. Hasa hushughulikia jinsi watu wanavyotumia lugha katika jamii.
Isimu- ni uchunguzi wa lugha kisayansi.
Jamii  ni kundi filani la watu wenye uhusianfulani.
Mambo yanayoshughulikiwa katika isimu jamii
i)   Tofauti katika lahaja za lugha kama vile Kiswahili cha lamu(kiamu), cha
Mombasa(kimvita), cha unguja(kiunguja), chbara.
ii Tofauti katika matumizi ya lugha baina ya makundi tofauti tofauti katika jamii. Mfano
wazee na watoto,vijana na wabunge.
iii) Matumizi ya lugha kutegemea miktadha tofauti kama vile kazini, nyumbani, sokoni, n.k.
iv) Mtazamo wa watu kuhuslugha. Je, wanaitukuza au wanaitweza?
v Jinsi mtanavyotumia lugha kutegemea uhusianna wazungumzaji au mada husika.
vi) Lahaja mbalimbali za lugha ya Kiswahili.
Umuhimu wa isimu jamii.
i)   Huwafunza watu kaida za lugha ili waweze kuitumia ipasavyo kutegemea mila na desturi.
ii Humsaidia mzungumzaji au mwandishi kutumilugha ya Kiswahili kwa ufasaha na usahihi.
iii) Humpa anayetumia lugha uwezo wa kutambua, kutofautisha na kutumimitindo mbalimbali ya lugha kutegemea mahitaji.
iv) Hufunza maadili ya jamii hasa yanayohusiana na matumizi ya lugha kutegemea uhusiano.
Mf. Mtu na mkwewe, mtoto na mzazi, mwajiri na mwajiriwa.
v Hufunza mbinu za mawasiliano pamoja na mbinu za kupata maana kamili. vi) Hudhihirisha utamaduni wa jamii.
vii) Humsaidia msemaji au mwandishi kutambua makosmbalimbali yanayojitokeza wakati wa kuzungumza au kuandika.
viii Hufunza mbinu za kuwaelewa watu tunaotagusana nao kwa kuzingatia mambo k.hadhi, utamaduni hivyo utangamano.
Maana ya mawasiliano.
Utaratibu ambao huwawezesha viumbe kupashana ujumbe ambao unahusisha mwasilishi na
mpokeaji wa ujumbe.
Njia ambazo kwazo mwanadamu huwasiliana.
i)    Mgusano na ukaribianaji ii Mavazi
iii) Sauti
iv) Ishara za mwili.
Lugha
Ni mfumo wa sauti za nasibu zinazotumiwa na wanadamu katika mawasiliano.
Sifa za lugha.
i)   Hakunlugha iliyo bora kushinda zingine. –zote ni sawa.
ii Kila lugha ina sifa zake.
iii) Lugha hubadilika kutegemea mazingira, aina ya tukio, wakati na matumizi ya lugha hiyo.
iv) Lugha ina uwezo kukua, mfano Kiswahili kimebuni msamiati TEHAM(Teknolojia ya habari na mawasiliano.)
v Lugha pia hufa kwa msamiati wake kupotea n.k
Sababu za kufa/kufifia kwa lugha.
(i) Lugha moja kusonewa hadhi na isiyoonewa hadhi hufifia.
(ii) Sababu za kiuchumi  watu huishi mijini na kuacha lugha ya kwanza.
(iii) Lugha kuwa na idadndogo ya wazungumzaji(iv) Ndoa za mseto.
(v) Kuhamia kwingine  watu huishi na kuingiliana na kundi jingine.
(vi) Mielekeo ya watu  wanapoipendelea lugha moja na kuidharau nyingine. (vii) Kisiasa  Lugha moja kupendelewa kuliko nyingine na viongozi.
Umuhimu wa lugha.
i)   Hutumika kwa mawasiliano.
ii Lugha ni chombo ambachhutusaidia kujieleza na kutoa mawazo yetu. iii) Hujenga uhusianbaina ya watu.
iv) Ni kitambulisho chtaifa, mtu binafsi na utamaduni.
v Lugha ni chemchemi ya uchumi mf. Mtangazaji au mwalimu wa Kiswahili.
vi) Huweza kuunganisha watu kama jamii moja.
Istilahi za Isimu Jamii
Lugha ni mfumo wa sauti unaochangia kw amawasiliano ya kimaeneo.
Msimbo  Huwa ni lugha ibuka ya kupanga ill kufichmaana.
Misimu  Ni lugha inayozungumzwa na kundi ndogo la watu katika jamii. Hasa huibua
misamiati mipya kila uchao.mf. toa chai, dondosha,
Diglosia  hali ya kuwa na lugha mbili tofauti katika taifa, zilizo na majukumu tofauti k.m
nchini Kenya Kiswahili ni lugha ya taifa, Kiingereza ni lugha ya ofisini/rasmi.
Polyglosia  hali ya kuwa na lugha nyingi tofauti(zaidi ya tatu) katika taifa, zilizo na majukumu
tofauti.
Lahaja ni vilugha ambavyo huzalishwa kutoka katika lugha moja kuu, kwa mfano lahaja za
Kiswahili ni kama; kiamu, kipate, kisiu, kijomvu, kimtangata, kiuguja n.k.
Lafudhi(accent)
Ni upekee wa mtu kuzungumza.
–   Lafudhi ni matamshi ya mzungumzaji yanayojitokeza kutokana na athari za lugha yake ya
kwanza, lugha zinazomzunguka au maumbile katika ala za sauti.
–   Mfano: rara badala ya lala, papa badala ya baba.
Sababu za kuwa na lafudhi.
(i)      Kwa sababu za athari ya lugha ya mama.
(ii)     Kwa sababu za athari ya lugha zingine zinazomzunguka mzungumzaji.
(iii)    Kwa sababu ya kasoro fulani iliyoko katika ala za matamshi za mzungumzaji.
Pijini.
Ni lugha ambayo huzuka katika shughuli za kibiashara au kidini baina au miongoni mwa
makundi yanayotoka maeneo mbalimbali.
Sifa.
·    Haina wazungumzaji asilia.
·    Huwa sahili na irabu za kawaida.
·    Haijakomaa kimsamiati.
·    Hukiuka kanuni za lugha.
·    Huwa haina wenyeji au wazungumzaji wazawa.
·    Hutumia ishara kwa sababu ya uhaba wa msamiati.
Krioli.
Ni pijini iliyoimarika na kuwa na watu wanayoizungumza kama lugha yao  ya kwanza
Eleza sifa zozote tatza krioli.
(i)   Huwa na wenyeji kwa mfano; Krioli ya Haiti, Kridi ya Jamaica
(ii Huwa na miundo thabiti ya kisarufi.
(iii) Huwa na msamiati shabiti unaoweza kutungiwa kamusi.
iv) Huwa na matumizi mapana katika Nyanja za siasa, muziki, vyombo vya habari na kadhalika.
Lugha mame
Ni lugha asiliambayo haijaathirika na ingali katika umbo lake asili
Mfano: kifaransa
Lugha azali ni lugha inayozaa lugha nyinginezo. Uwili lugha uwezo wa mtu kuzungumza lugha mbili. Sababu zinazochangia kuwepo kwa uwingi lugha.
i)    Ndoa za mseto
ii)   Ujirani wa makabila / mataifa tofauti iii Sera za lugha za wakoloni.
iv)  Sera za lugha za nchi.lugha rasmi na lugha ya taifa huweza kuwa tofauti.
v)   Mavamizi / vithuwalazimu wananchi kuhamia kwingine hivyo kuwafanya kujifunzlugha
geni. vi Dini vii) Elimu
viii) Umataifa / udiplomasia
ix)  Uchumi na biashara
ix) Mwingiliano wa watu katika jamii.
Aina za uwililugha
a)  Uwililugha sawia
Hii ni hali ya kuwa na uwezo wa kuzimudu zile lugha mbili
b)  Uwililugha kupendelea
Ni hali ya kuwa na mwegemeo wa kuionea fahari mojawapo ya lugha unazozijua
c)  Uwililugha kupokea
Hii ni hali ya kujibu lugha moja kutumia nyingine, kwa mfano mtoto anapozungumziwa kiingereza akajibu kwa Kiswahili
d)  Uwililugha uliolala
Ni hali ya kuwa ugenini na kulazimika kuisahau lugha yake kwa muda.
e)  Uwililugha mfu
Ni hali ya lugha moja kumezwa au kufifia na kutotumika tena.
Eleza maana ya Lingua Franka.
Ni lugha inayotumiwa na watu walio na lugha tofauti kwa ajili ya mawasiliano kwa mfano
Kiswahili katika eneo la Afrika Mashariki.
Sif za Lingua Franka.
   Huwa ni lugha ua mawasiliano kati ya watu wenye lugha zaidi ya moja.
     Yaweza kuwa lugha ya kwanza ya mzungumzaji au lugha ya pili na kwa watu wenginlugha ua kigeni
   Hukiuka mipaka ya kitamaduni
   Hukutanisha watu wa asili mbalimbali.
   Hukiuka mipaka ua kimaeneo – inaweza kutumiwa katika maeneo mapana.
   Hutumiwa na watu ambao lugha zao za mama ni tofauti.
Umuhimu wa lingua franka
–     Huleta ushirikiano katika nyanja mbalimbali kama vile, kibiashara, kiuchumi, kielimu, kidini
nk
–     Huleta umoja miongoni mwa watumiaji wake hasa wale wenye tamaduni tofauti
–     Hurahisisha mawasiliano hasa katika jamii inayogawika katika misingi ya lugha.
Njia za uzambazaji wa linguafranka

(i)     Vita kwa mfano lugha ya kigiriki iliweza kueneza kupitia vita. Kifaransa pia kilienezwa kupitia vita hasa wakati wa utawala wa Napoleon Bornaparte
(ii)    Biashara kisawhili kimeweza kuenea kutokana na dhima yake katika biashara
(iii)   Ukoloni kifaransa, kiingereza na kireno zimeweza kuenea kupitia utawala kama nyenzo
(iv)   Elimu- lugha kama kiingereza zimeweza kuenezwa kwa kutumika kwenymafunzo katika nchi nyingi za ulimwengu
(v)    Nguvu za kisayansi na teknolojia Nguvu za kisayansi na teknolojia za Amerika zimechangia kuenea kwa kiingereza katika ulimwengu hasa kwa sababu ya istilahi mpyzinazoibika kila uchao.
Misimu semi za mda zinazotumika na kikundi fulani cha watu na hutoweka kwa baada ya mda.
Eleza tofauti kati ya kuchanganya ndimi na kuhamisha ndimi.
i). Kuchanganya ndimi  hali ya kutumia zaidi ya lugha moja katika mawasiliano . matumizi
haya hujikita katika sentensi moja / mzungumzaji anatoka kidogo katika lugha moja na kuingilia nyingine kasha akarejelea lugha awali.
ii)Kuhamisha ndimi  kubadilisha mkondo wa mazungumzo kutoka lugha moja hadi nyingine ambapo msemaji anumilisi wa zaidi ya lugha mbili.
Andika sababu nne za kuchanganya na kuhamisha ndimi.
   Kupungukiwa na msamiati wa kutumia
   Kujitambulisha na kundi fulani la watu mf waliosoma, wanahirimu n.k
   Kujihusisha na lugha inayoenewa fahari
   Kutaka kuonyesha kuwa una uwezo wa kutumia lugha mbili au zaidi
   Kutaka kufafanua dhana fulani k.m uyoka (x-ray)
Huku ukitoa mifano mwafaka, fafanua kaida tano katika jamii ambazo matumizi ya lugha hutegemea.
.
(i)        Mazingira/muktadha.
Hutegemea mazingira ya wazungumzaji k.v. ofisi, sokoni, mahakamani,
kanisani n.k.
(ii)       Umri
Vijana wana namna ya kutumilugha inayojihusisha na mitindo mipya tofauti na wazee wanaotumia msamiati wenye hekima na ushauri
(iii)     Uhusiano
Kuna mahusiano ya aina nyingi, kwa mfano mtoto atatumia lugha kwa njia tofauti katika kuwasiliana na wazazi wake tofauti na vile atazungumza na watoto wa rika lake
(iv)      Jinsia/ uana
Unyenyekevu hujitokeza katika mazungumzo ya wanawake ambayo ni tofauti nay a wanaume. Lugha ya wanaume huwa na fujo, kiburi na hali ya kutojali sana. Wanawake watajikita katika mapambo ilhali wanaumewatajikita katika siasa.
(v)       Madhumuni/lengo.
Lengo la mzungumzaji humlazimu kuchagua mtindo atakaoutumia kuufikisha ujumbe wake.
(vi)      Mada
Swala linalozungumziwa hulazimu mtu kuteua msamiati unaohusiana na mada yenyewe.
Kwa mfano, iwapo ni kuhusu kilimo, msamiati wa ukulima utatamalaki mazungumzo
(vii)     Hali ya mtu

Mgonjwa atazungumza kwa upole wakati mlevi atazungumza kiholela bila kuchagumaneno
(viii)   Cheo cha mtu/ hadhi
Madaraka ya mthuchangia msamiati wa kutumia. Hali ya kuamuru hujitokeza katika lugha ya waajiri ilhali upole na adabu hutumiwa na waajiriwa.
(ix)      Utabaka
Hadhi ya mzungumzaji inaweza kuathiri uchaguzi wa msamiati.
Watu wa tabaka la juu watapenda kuchagua maneno ya kifahari ilhali wale wa tabaka
la chini watatumia maneno ya kawaida.
TANBIHI: Kaida katika matumizi ya lugha husababisha kuwepo kwa sajili tofautitofauti katika
miktadha mbalimbali.
Sajili za isimujamii
Katika isimujamii, kuna sajili ainati ambazo zina sifa za kipekee ambazo huwa na umuhimu wake k.m.
Sajili ya mahakamani
Sajili ya biashara
Sajili ya maabadi
Sajili ya mtaani/vijana
Sajili ya hospitali Sajili ya kitaaluma Sajili ya nyumbani Sajili ya biashara.
Sajili ya matangazo ya mpira
Sajili ya bungeni.
i.         Sajili ya mahakamani
Soma kifungu kifutacho:
Kwa mujibu wa sheria kifungu nambari 3 sehemu ya ya sheria za nchi, umepatikana na hatiya kutatiza utulivu wa raia wapenda amani kwa kuwatusi na kutisha kuwapiga. Kiongozi wa mashtaka amethibitisha haya kwa kuwaleta mashahidi ambao wametoa ushahidi usiotetereka kuhusu vitendo vyako katika tukio hilo. Korti hii imeonelea una hatia na imeamuru ufungwe jela kwa muda wa miaka miwili bila faini ili liwe funzo kwako na kwa wenzako wenye tabia kama zako. Una majuma mawili kukata rufani.
Sifa za sajili hii
a.   Msamiati teuleJela,rafani,mashtaka,sheria, kiongozi wa mashtaka, mashahidi,
Hakimjaji, mhalifu,Washikadau / wahusika  kwa mfanb.   Sentensi ni ndefundefu kimuundo.
c.   Kurejelea vifungu vysheria za nchi. d.  Lugha ya hakimu niya kuamuru.
e.   Matumizi ya lugha ya heshima/unyenyekevu mf mheshimiwa kurejelea jajif.   Matumizi ya maneno ya kukopa/kigeni mf nole proseque, amicus curie nk.
g.  Lugha rasmi hutumika.
h.   Lugha dadisi hutumika haswa pale mwendesha mashtaka humhoji mshukiwa.
i.    Lugha sanifu imetumika kila neno linalotoka kinywani na muundo wa sentenshuwa na umuhimu wake katika kesi.
j.    Lugha iliyotumika ni ya mfululizo – Hakimu anapotoa hukumu hakatizwi.
Sajili ya darasani/shuleni/ofisi shuleni.
(i Sentensi ndefu  (atoe mifano katika hoja zote.(ii) Huwa na mwanzilishi mkuu.
(iii)Misamiati ya taaluma mbalimbali(iv) kurejelea mawazo ya wengine.

(v) Lugha ya heshima/adabu. (vi) Kuna urasmi wa lugha
(vii Lugha iliyo na mbinu au ataratibu maalum;kwanza,kuongezea na mwisho kabisa....
Sajili ya biashara.
Ponda mali:                  Karibu! Wamama wangare mali safi ambayo huwezi kupata
popote duniani.
Amina:                          Unauzaje hilo rinda?
Ponda mali:                   Bei ni kusikilizana, hatuwezi kukosana.
Amina:                          Nitakupaa shilling hamsini, naona ni mtumba.
Ponda mali:                   Mama hilo rinda ni original kutoka Marekani kwa meli.
Amina:                          Nitaongeza shilingi kumi basi.
Ponda mali:                   Ongeza kidogo, usiniue.
Sifa.
(i Inaeleza ubora wa bidhaa.
(ii) Kuna kupiga chuku k.m huwezi kupata popote duniani(iii)Ina ushawishi.
(iv) Haizingatii kanuni za sarufi  wamama. (v) Kuchanganya ndimi  original.
(vi) Hutumia lugha ya mkato. (vii)    Hujaa porojo.
(viii) Hutumia lugha nyepesi.
Sajilkatika muktadha wa usafiri.
Aziz:         Ingia 46! Adams mbao Kenyatta, railways beba! 46 Adams mbao Kenyatta, railways!
Shiku:       Nambnane ngapiAziz:         Mbao ingia, blue.
Shiku:       Nina hashuu
Aziz:         Blue Auntie
Shiku:       Sina
Aziz:         Ingia. 46 Adams mbao, Kenyatta railways gari bebabeba.
Ahendera: Mimi sinako shirini. Chukuako tu kumiAziz:         Dinga inakunywanga petrol mzee. Ahendera: Kumi mingi.
Aziz:         Haaya ingitwende. Dere imeshona twende. Beba mbele.
Sifa
i.    Kuna matumizi ya lugha maalum k.v 46, ingitwende.
ii Kuna kitaja vituo mbalimbali ambako gari litapitia. iii. Ni lugha ya kuchanganya ndimi k.v driver
iv Inatumia misimu k.hashru, dinga n.k
v.   Haizingatii sarufi k.m inakunywanga, sinako n.k
vi Hutumia sentensi fupifupi vii. Ina ucheshi mwingi.
Sajilkatika kituo cha polisi.
Ali:   Wee kuja hapa.  Wewe ni nani? Sema haraka
Ebo: Mimi  ni  afande ni Ebo
Ali:    Unatoka wapi sa ii? Hapa hakuna sheria?
 Ebo Samahani mkubwa. Mimi niku…
Ali:    Mkubwa wa nani? Wakubwa wako ofisini.
Sifa.

Ebo Pole mzee.
Ali:     Mzee gani? Hii mtu lazima niiwekwa store. Yaani selfcontained.
Toa viatu.
Ebo Tafadhali Bwana Askari, nilichelewa 
Ali:     Mimi sitakhadithi! Hizo pelekea nyanya yako, eh Fanya haraka!
Ebo:   Naomba mkubwa 
Ali:      Hapa si kanisani. Unaomba! Hata 

   Lugha yenye ukali kw. Polisi.
   Lugha ya kudhadisi/maswali ni majibu.
   Kuchanganya ndimi.
   Lugha isiyozingatia kanuni za kisarufi.
   Lugha ya unyenyekevu kwa mshukiwa.
   Lugha ya kuamrisha.
   Lugha inayoeleweka kwa urahisi
   Lugha ya misimu.
Sajili ya maabadini.
Ndugu na madada, sote tumealikwa katika karamu hii ya Bwana kabla ya kujongea mezani pake, Bwana.   Pana haja ya kutakasa nyoyo zetu na kujutia madhambi yetu.   Sisi sote ni
watenda dhambi na inastahili kumwendea ili aweze kutuondolea madhambi yetu.
Sifa.
(i)
Matumizi ya msamiati maalum kwa mfano:
Mungu asifiwe.
Biblia.
Alhadulillahi!
Shetani ashindwe!
(ii)
(iii)
Matumizi ya sentensi refu ili kuweza kueleweka vizuri na waamini.
Matumizi ya ukale wa lughajinsi ilivyoandikwa.
(iv)
(v)
Kudondoa kauli yaani kurejelea sehemu fulani katika maandiko matakatifu.
Uradidi wa maneno kurudiarudia maneno kama:
Mungu yu mwema
Mwenyezi Mungu
(vi)
Amina n.k.
Matumizi ya ishara na miondoko.
Anapohubiri hutumia ishara na miondoko mfano kuinua mkono, Kuruka kutoka
hapa na pale.
(vii)
Kuchanganya nyakati sana kwa mfano: naye akaondoka hapo waende upande wa
mashariki.
(viii)
Matumizi ya maneno yenye asili ya kigeni kwa mfano: majina ya wahusika Sila
na Petero.
(ix)
(x)
Matumizi ya lugha maalum kama vile tamathali za usemitaswira, jazanda n.k.
Mwelekeo mkubwa wa kunukuu vifungu kutoka vitabu vitakatifu k.v Biblia na
Koran
Sajili ya hospitali.
KCSE 2010
Benki yenyewe haina kitu ... CD4 count yake iko chini ... Ni emergency ... Tutampoteza ikikosekana.
(a) Taja sajili inayorejelewa na maneno haya. (alama 2)

Sajili ya hospitali/hospitalini/matibabu/kituo cha ya
/zahanati/udaktari/uuguzi/uganga/uganguzi/utabibu/tiba/daktari/tabibu
(b) Fafanua sifa nne zinazohusishwa na sajili hiyo. (alama 8)
i) Kuna matumizi ya msamiati maalum/maneno teule ya kunywa mara mbili x3/uyoka/exrei/machela n.k
ii) Matumizi ya vifupisho mf CD4/v.c.t
iii) Matumizi ya lugha mseto/kuchanganya ndimi
iv) Kubadili au kuhamisha ili kufanyiwa msingo.
v) Kuna kudadisi/kuuliza maswali/kuhoji/mahojiano/Dayolojia/kusaili/majibizano
m.f Daktari: ulianza kuugua lini? Mgonjwa:
vi) Kutohoa oparesheni benki
vii) Matumizi ya kaulfupifupi/sentensi fupifupi/lugha ya mtaa mf. jina lako? Umri wako?
viii) Matumizi ya lugha maagizo/Tahadhari/masharti/kuliwaza/ushawishi/ unyenyekevu/
ushauri mf.usitumie pombe
ix) Manenhuwekwa wazi/lugha ya ufafanuzi/maelezo ya ndani zaidi mf. Nilipata
ugonjwa kutoka umalaya.
x) Lugha ya usiri m.f Daktari/madaktari huwa na lugha yao isiyoeleweka na
mgonjwa/lugha fiche/matumizi ya mafumbo. xi) Kuna lugha ya kitaaluma mf CD4 count
xii) Wahusika hurejei wa kwa majina au vyeomf. Bw Daktari
xiii) Matumizi ya lugha ya hisia, mf mgonjwa kutoa usiahi kwa sababu ya maumivu.
xiv) Lugha ya mdokezo ulisema ulianza. xv) Lugha ya matumizi ya usemi halisi
xvi) Matumizi ya lugha ya kwa moja/ana kwa ana
xvii) Matumizi ya ishara/miche 1 x 1/hisabu picha au alama n.k
Sajilkatika muktadha wa siasa.
Wananchi mimi  sina  mengi Hapana  katika  nyinyi  asiyenielewa.  Sina  l kusema,  ila
ninawakumbusheni kuwa mnahitaji kiongozi atakayeshughulikimaslahi ya taifa zima.  Mthuyo ni mimi na ninajitahidi niwezavyo kujenga masoko, barabara, shule zaidi na mazahanatna maisha yenu yatakuwa ya raha zaidi.
Sifa.
i.     Imejaa propaganda k.v. Fulani ni muaji ( bila idhibati)
ii.    Ina ucheshi mwingi k.v. rais na mpira aingize bao
iii.   Lugha imejaa mafumbo. Yaani ni fiche k.v. ina vitendawili vinategwa iv.   Istilahi maalum k.v kura, mgombea. Demokrasia, katiba
v.    Lugha huzingatia mbinu za tawasifu- majisifu kuhusmatendo bora ya mtu.
vi.   Lugha shawishi inayovutia wafuasi wengi k.v tafadhali nawasihi mnipigie kura
vii.  Inchuku k.v ahadi nyingi zisizoweza kutimizwa zote
viii. Mjadala uwepo wakati mwingine.
ix.   Huweza kuchanganya ndimi kwa kutumilugha mbalimbalix.    Mara nyingi sarufi haizingatiwi.
xi.   Huwa na kukatizana kauli kutokana na kupiga makofi, vigelegele au kutokubaliana kwa kauli Fulani.
xii Lugha yenye matusi hasa wanaporejelea maadui/wapinzani wao. xiii. Msamiati wa heshima hutumika haswa wanaporejelea wananchi.
Sajili ya bungeni
...napinga hoja iliyotolewa na waziri wa Finance ya kupiga marufuku matumizi ya plastibags Baada ya kumsikiza kwa makini, ningependa kumkosoa kwa kudhihirisha kuwa...
kulingana na kifungu nambari 
Sifa.

i.    Kuchanganya msimbo/ndimi katika mijadala, ili kujieleza vyema  waziri wa Finance. ii Lugha ya adabu  naingependa kumkosoa.
iii Msamiati na istilahi huhusiana na bungeni k.m. vikao vybunge, spika, mesi, karani 
hoja, kifungu nambari n.k.
iv Hurejelea sheria za nchi au katiba katika kutetea hoja fulani inayojadliwa.
v.   Lugha ya heshima katika mawasiliano na majadilianoMheshimiwa spika
vi Wabunge hutaja msamiati unaorejelea sheria na kanuni za bunge wanapojadiliana

kuhusiana na maswala mbali mbali

hasa shughuli za kinidhamu. vii. Lugha huwa sanifu.
viii.           Huwa na urudiaji wa manenmfano. Bwana Spika.
ix Huwa na kukatizana usemi mfano palambapo mbunge husimama kwa hoja ya nidhamu.
x.   Mara nyingi huwa na sentensi ndefu ndefu.
Sajili ya hotelini.
Nani kuku..? Sosi poleo ...... Mate ndo! ndo! ndo!. Ukimanga hii hutaona daktari kwa miaka
kumi…... Ngombe je? nani? …...nani!... Ni wewe....... pobasi naja............
Sifa.
i.     Matumizi ya maneno au kauli ambazo katik mazingirmengine haziwezi kuwa nmaana nani kuku?
ii.    Ngombe je?
iii.   Matumizi ya msamiati maalumu wa hotelini kwa mfano,
i) Karanga     ii) Ngombe iii) Chipo             iv) Chapo iv.   Lugha ya ucheshi na utani
v.    Matumizi ya misimu   ukikimanga / surwa vi.   Kuchanganya ndimi
vii Lugha isiyo sanifu k.m Ukimanga viii. Tanakali km. matndo..ndo..ndo...
ix.   Matumizi ya sentensi fupi fupi.
Sajili ya simu
ahnaomba kumwongelesha Chucho...Naam, naam Chucho
Hujambo?…si sina nenonaam. Mjomba amezidiwa si wa maji si wa chakula...
kweli?...Muuguzi mkuu amedhihirisha...Yes...ok...yeahAla! Ameishiwa na pesa.
sifa za sajili hii.
i.     Hutumai sentensi fupifupi ili kuokoa wakati mf. Naam
ii.    Huendeleza majibizano mf. Majibizano kati ya Chuchna anayepiwa simu. iii.   Hutumia mbinu ya takriri mf. Chucho, naam
iv.   Huhusisha kuchanganya ndimi mf. Kiingereza yes, yeah
v.    Aghalabu kanuni za lugha hukiukwa mf. Kumwongelesha
vi.   Hulenga moja kwa moja kiini cha habari k.m. Baada ya maamkuzi, anamweleza kuhussiha ya mjomba moja kwa moja.
vii Kukatana kalima
viii. Matumizi ya maamkuzi
Sajili ya michezo.
Anachukua ile ngoma kijana RooneyKwake chicharito...anachenga moja , mbili
Hatari! Hatari! Hatari kwenylango

Sifa.

i.    Kuna kuchanganya ndimi na kubadilisha ndimi.


ii.  Matumizi ya msamiati maalum wa michezo. iii. Hukiuka kanuni za kisarufi/ kuiboronga sarufi iv. Hutumia mbinu ya utohozi.
v.  Matumizi ya lugha ya mkato
vi. Matumizi ya uradidi wa maneno au kauli fulani
vii. Matumizi ya misimu.
viii.     Matumizi ya lugha ya taharuki.
ix. Matumizi ya majisifu mengi
x.   Kuna kutajataja majina ya wachezaji.
Sajili ya matangazo/ habari/ripoti/radio.
Mfanyikazi mmoja wa nyumbani amefikishwa mahakamani katika kaunti ya Maganyakulo
kujibu tuhuma za kumbaka kikongwe. Mwendesha mashtaka wa polisi bwana Maliza Twende alisema. Mikaka na Makarne alifumaniwa na mshtakiwa alipelekwa rumande hadi septemba 21 mwaka huu ambapo kesi hiyo itatajwtena. Licha ya hayo, wengi wanadokeza kuwa Huenda adhabu ya kosa hilo ikuwa ni kifo au kifungu cha maisha. Mshtakiwa aliomba apewe dhamana na Serikali ili aachiliwe huru. Hatimaye ombi hilo halikukubaliwa kwa kuwa mfanyikazi huyo hakuwa na mdhamini. Muhimu ni kuwa baada ya kesi hiyo kuamuliwa, mshtakiwa anaweza kukata rufaa katika mahakama kuu. Naye mlalamishi ameomba Serikali impe ulinzi kutokana na kuvamiwa na washirika wa mshtakiwa
Sifa.
i.   Huwa na lugha nyepesi
ii.  Sentensi aghalabu huwa ndefu ndefu
iii. Hufuata kanuni za usarufi wa lugha
iv. Huhusisha maelezo ya kina ili kuweka wazi yaliyojiri
v.  Mara nyingi hutumia wakati uliopita
vi. Wakati mwingine huhusisha wadhamini.
Sajili ya magazetini.
ya leo ni kuwapa pole wanaofuata na kuenzi makala ya Burudani,toleo la kila
Ijumaa.Mwanamziki huyu aliteka nyoyo za wapenzi wa mtindo huu wa mziki.Kwa kweli ya
Muumba hufumbwa tu!Mnapoyasoma wakumbukeni jamaa na wapenzi wa nyimbo zake.
Sifa.
i.    Hutumia usemi halisi sana ii Huchanganya njeo.
iii. Huchanganya ndimi.
iv Hutumia vifupishoShirika la REUTERS.
v.   Lugha hupiga chuku
vi Wakati mwingine husheheni sifa.
Sajili ya vijana.
Niaje wasee! Maholiday ndizo hizo tena. Najua mamission ni mingi! Lakini jo !
Mambo imebadilika ! Ni kubaya maze. Usifikirikil kitu unaona ni reality, ukadhani ni
gold ! Hiyo siyo real life maze ! Round hii maze ni Kuchill!’ Usipige  mastuntzingine zitakuacha uki-regret later! NI POA KU- CHILL au aje maze?

sifa

i.    Kubadilisha msimbo –usifikirie kila kitu unaona ni reality.
ii Si lugha sanifuNajua mamission ni nyingi lakini jo, mambo imebadilika iii. Matumizi ya sheng-    Mamission
a.   Kuchill
b.   Uki-regret
iv Matumizi ya sentensi fupi–    Ni kibaya maze
i.   Ni poa kuchill


v.   Kuchanganya msimoKuchill ;Ukiregret ;Mamission. vi Kuna kukatizana kauli.
Sababu za vijana kutumia lugha hii.
i.    Ukosefu wa msamiati.
ii Kukubalika katika kikundi fulani.
iii. Kujitambulisha na lugha fulani au kuonyesha umahiri katika lugha zote mbiliiv Kufahamu lugha zaidi ya moja.
v.   Sheng` ni lugha legevu(rahisi).
vi Kuipa lugha ladha(kiswahili sanifu hakina ladha)
vii. Ili kuficha ujumbe.
viii. Kujitambulisha na wanahirimu.
Sifa za sheng`
i.    Huwa na msamiati maalumu unaotumiwa na vikundi vya watu wenye sifa au tabia fulani. ii Hujumuisha maneno mapya na maneno ya kawaida.
iii. Aghalabhaijali sheria za kisarufi.
iv Msamiati wake huwa finyna chakavu.
v.   Manenhusika hupewa maana mpya zilizo tofauti na zile zilizozoeleka katika lugha nyingine.
vi Aghalabhuwa mchanganyingo wa lugha nyingi. vii. Kuna ufupishaji wa maneno na sentensi
Sifa zinazoifanya lugha ya sheng` isiwe lugha ya taifa.
i.    Kubadilikabadilika kwa msamiati.
ii Si lugha sanifu.
iii. Haizungumziwi na watu wengi
iv Hasa ni vijana
v.   Sio lugha ya mama ya kikundi Fulani katika nchi
vi Basi haitajulikana kwa urahisi.
vii. Muundo haufananai na baadhi ya lugha za kwanza za kabila Fulani.
viii. Si lugha ya kienyenji.
Athari za Sheng
1.  Huweza kuathiri namna mwanafunzi anavyojieleza katika mahojiano ya kazi.
2.  Kukuza matumizi ya lugha legevu katika maongezi na maandishi.
3.  Kupotosha ujumbe km. pesa pap!
4.  Kielelezo kibaya kwa jamii nan chi kwa ujumla km. kuonyesha nchi isiyo na sera bora ylugha.
5.  Ni njia ya kufifisha uzalendo wa kujivunia lugha ya taifa.
6.  Ni msimbo wa kuficha maovu. Inaweza kutumiwa na vijana kutekeleza maovu.  km una mozo/unga (sigara)
7.  Huchangia katika alama duni kwa mtihani.
Sajili ya mazishi /matanga /kilio masikitiko /msiba/ maombolezo/uzikaji.
sote tunajua kwamba ni kudura. makiwa!
Sifa
i.    Msamiati maalum kwa mfano makiwa marehemu.
ii Lugha ya kufariji/liwaza iii. Yenye matumaini
iv Matumizi ya vihihisishi oh, wuuiv.   Lugha ya kusitasita
vi Huhusisha sana mambo ya kidini na Mungu na Imani za jamii.

vii. Ni lugha ya hasira. viii. Kuchanganya ndimi
ix Inaadaman na viziada lugha
x.   Matumizi ya sentensi fupi
xi Matummizi ya sentensi ndefu
xii. Imesheheni sifa za m wendazake
xiii. Matumizi ya lugha isiyozingatia kanuni za kisarufi.
Hadhi ya lugha. Lugha rasmi.
Ni lugha inayopewjukumla kutumika kikazi mf katika kuendeleza shughuli rasmi k.v elimu, utawaln.k.
Sifa.
·    Hutumika katika mazingira au shughuli rasmi kv. Mikutano ya mawaziri,elimu, mikutanya machifu n.k
·    Aghalabhuwa ni lugha inayosemwa nchini na pia nje ya nchi. Mf. Kiswahili.
·    Inaweza kuwa lugha mojawapo ya wenyeji au lugha ya kigeni.
·    Yaweza kutekeleza majukumu mengine k.v kuwa lugha ya Taifa.
·    Huwa imesanifishwa na kusambazwa kupitia vyombo vya habari, vitabu na machapishmengine.
·    Mara nyingi huwa ni lugha yenye historia ndefu.
·    Iweze kutoa fursa ya kujiendeleza kimsamiati kutokana na kuibuka kwa maneno mapya.
·    Huwa na msamiati mpana katika kila Nyanja za maisha. Isikosekane fasiri ya neno katika lugha hiyo.

Sifa za lugha ya taifa
·    Ina wazungumzaji wengi.
·    Ina uwezo wa kutoa hisia za kikabila na kuwafunza watu kuhisi kuwa taifa moja.
·    Huwapa watu utambulisho katika umoja wa mataifa.
·    Huibua hisia za kizalendo miongoni mwa wananchi.
·    Ni lugha ya mama/ kwanza ya kikundi cha watu katika taifa husika
o Ili wapokezane utamaduni, amali na historia.
o Ili wafunze wengine
·    Iwe na muundo wa kiisimu unaofanana na ule wa baadhi ya lugha za watu katika taifhusika hivyo kujifunza ni rahisi k.m Kiswahili na lugha zingine za kibantu K.v kiluhya ,
Kikuyu n.k
·    Iwe lugha mojawapo asilia, isiwe ya kigeni bali ya kienyeji; isilete chuki bali ieleze hisia za uzalendo na utaifa.
Majukumu.
·    Huunganisha watu wa taifa/huleta umoja.
·    Huziba mipaka ya kikabila.
·    Hukuza utamaduni wa kiafrika.
·    Hukuza uzalendo wa watu wa taifa kwa kutumilugha kama kifaa cha kuonyesha hisia za kizalendo.
·    Hutambulisha watu wa taifa fulani kwa mfano; wimbo wa taifa n.k.
·    Huleta maendeleo ya kijamii, kisiasa, kiuchumi na kisayansi kutokana na umoja wa taifzimkilugha.
·    Hufanikisha harakati za uongozi.
·    Husawazisha watu kilugha kwa sababu hisia zitakuwa sawa.
Lugha ya kimataifa.
Ni lugha ambayo inaweza kutumika katika mawasiliano nje ya mipaka ya nchi husika kwa masuala ya kisiasa, kidiplomasia, kibiashara na kitamaduni.
Sifa za lugha ya kimataifa.
·    Ina uwezo wa kutimiza masualya kidiplomasia, kiuchumi, kisiasa, kielimu na hata sera katika nchi mbalimbali.
·    Ina uwezo wa kutumika katika vyombo vingi vyhabari katika pembe nyingi duniani.
·    Ina uwezo wa kutumika katika utafiti na uchunguzi kote duniani.
·    Inasemwa katika pembe nyingin za dunia na watu wengi.
·    Inatumika kuendesha mikutanna shughuli rasmi za kimataifa.
Majukumu ya lugha ya kimataifa.
·    Hufundishwa katika vyuo vikuu vingi duniani Amerika, Ujerumani, Uswidi, Uingereza, Japani.
·    Hutumika kutangazia na idhaa nyingi duniani kuanzihapa Afrika ya masharikiUingereza kuna BBC, voice of Amerika, Radio Urusi, Radio China kimataifa n.k.
·    Kinasemwa katika kila pembe ya dunia mf. Afrika nzima, Amerika, China n.k
·    Ni kati ya lugha mojawapo ya lugha zinazotumiwa kama lugha rasmi katikumaja wa
Afrika(AU).

·    Hutumiwa katika kutolea magazeti mengi na majarida katika pembe tofauti za dunia.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *