1. Irabu / Vokali
/a/, /e/, /i/, /o/, /u/.
/a/, /e/, /i/, /o/, /u/.
2. Konsonanti
/b/, /ch/, /d/, /dh/, /f/, /g/, /gh/, /h/, /j/, /k/, /l/, /m/, /n/, /ng’/, /ny/, /p/, /r/, /s/, /sh/, /t/, /th/, /v/, /w/, /y/ na /z/.
/b/, /ch/, /d/, /dh/, /f/, /g/, /gh/, /h/, /j/, /k/, /l/, /m/, /n/, /ng’/, /ny/, /p/, /r/, /s/, /sh/, /t/, /th/, /v/, /w/, /y/ na /z/.
Tanbihi:
Sauti /q/ na /x/ hazijumuishwi miongoni mwa sauti za KISWAHILI.
Sauti /q/ na /x/ hazijumuishwi miongoni mwa sauti za KISWAHILI.
Irabu / Vokali hutamkwa kwa ulaini; bila kubana mkondohewa. Aghalabu mdomo huwa wazi au katika hali ya mviringo.
Sauti hizi hutamkwa kwa kutegemea hali au mkao wa mdomo, mwinuko wa ulimi au sehemu za kutamkia katika ulimi.
Sauti hizi hutamkwa kwa kutegemea hali au mkao wa mdomo, mwinuko wa ulimi au sehemu za kutamkia katika ulimi.
Konsonanti hutamkwa kwa kubana au kuzuia hewa katika ala za kutamkia. Sauti za Konsonanti ni ishirini na tano jinsi nilivyoorodhesha hapo awali. Sauti hizi huainishwa kwa kuzingatia:
Namna/jinsi ya kutamka,
Mahali pa kutamkia,
Mtikiso wa nyusi za kutamkia.
Sauti Ghuna na Sauti Sighuna
Katika lugha ya Kiswahili, kunazo sauti ghuna na sauti sighuna.
Ughuna wa sauti ni mrindimo au mtikisho unaoletwa na mtetemo wa nyuzi za sauti zipatikanazo kooni.
Sauti ghuna ni ile inayotetemesha koo wakati wa matamshi. Sauti ghuna ni nzito zinapotamkwa. Mifano ya sauti
ghuna katika Kiswahili ni:
b, d, g,v,dh, z, j, mb, nd na ng
Sauti sighuna ni sauti zitamkwazo bila ya mtetemeko au mrindimo wowote wa nyuzi za sauti. Ni hafifu zinapotamkwa.
Mifano ya sauti sighuna ni:
p,t,k, ch, f, th, s na sh