VITATE

VITATE
lugha na isimu,itv tanzania,chomoka na global,latest news kenya,renaissance,tanzania,citizen news,hiran mugaisi,michel bakenda,itv daima,capital fm kenya,one,aime nkanu,itv habari,citizen tv,felix tshisekedi,palinyang billy gabriel,cgtn africa,breaking news kenya,daily nation,standard news,wasafi,standard media,fr patrice ngoy,capital fm news,america,connect,trace tv,global tv online,fabregas,jb mpiana,ipp media,hivisasa

Vitate ni maneno yanayotatanisha kwa sababu ya ukaribu uliopo kimatamshi na kimaendelezo baina yake.
Mifano ya vitate:
Wasiwasi-jakamoyo, wahaka au shaka.
Waziwazi-bila ya kuficha.
Dhamini-wekea mtu ahadi kuwa utatimiza jambo fulani.
Thamini-tia maanani au heshimu.K.m Asiyekujua hakuthamini.
Bamba-lazimisha mtu kufanya ngono naye.
Pamba -chakula cha wakati wa safari.
            -tia urembo au visha mavazi mazuri na ya kupendeza.
Bali-isipokuwa, lakini, ila.
          -tia maanani.K.m sijali wala sibali atakayosema
          -herini.
Bari-jitenge,kaa kando
Mbali-masafa marefu baina ya mahali na mahali,
          hatua kwa hatua au mwendo mrefu.Pia umbali.
         -sio sawasawa.Pia tofauti k.m shati hili lina rangi mbali na lile.
         -Kwa kitambo kirefu k.m Amekwenda mbali.
Mbari -Watu wa kitovu kimoja.Kabila au ukoo.
Chini -Kinyume cha juu.
         -ndani ya ardhi,pango au meli.
        -sehemu ya mbele kinenani.Pia tupu.
Sini-udongo maalum wa kutengeneza vyombo.
      -asilani! au abadani!
Zini -kutenda tendo la kujamiana bila kufuata taratibu za kidini
Bua-shina la mtama au mhindi.
       -hutumika katika usemi: moyo wa bua-moyo unaotishika kwa wepesi.
       -chuma cha wahunzi cha kukolezea moto.
Pua-paka kitu kiowevu mwilini kwa kutandaza kiganja cha mkono.
      -maliza yote bila kubakisha kitu.
      -kiungo cha mnyama chenye tundu kinachomwezesha kuvuta pumzi na kunusia.
Fua-tengeneza kitu kutokana na madini.Pia sana.
      -,safisha nguo kwa maji na sabuni.
      -chano.
Vua-ondoa mwilini kitu kilichovaliwa.
      -toa katika matatizo.Pia nusuru.
Chaka -mahali penye miti iliyosongamana.
           -msimu wa kaskazi.
Shaka -hali ya kutokuwa na hakika ya jambo.Pia wasiwasi.
Posa-peleka maombi ya kutaka kuoa kwa wazazi wa binti.
Poza-malipo ya kumtuliza mtu kwa jambo baya alilotendewa.
Saka-tafuta mtu au mnyama ili kumkamata.Pia winda.
Zaka -moja ya kumi ya pato ambalo waumini wa baadhi ya madhehebu ya Ukristo hutarajiwa kutoa kwa ajili ya
         shughuli za kanisa.

Suka-fuma kitu ili kupata mfumo fulani ulioshikamana.
Shuka-teremka
Zuka-Anza au tokea kwa kitu au jambo ambalo halikuwepo wala kutegemewa.
Joshi-kwa haraka k.m dau la mnyonge haliendi joshi.
        -mwendo wa chombo wa kufuata upepo wa katikati
Jozi-vitu viwili vilivyopamoja na vinavyofanana.
Chozi-tone la maji au uowevu linalotoka machoni mtu anapolia au moshi unapoingia machoni
Tosa-tia kitu katika kiowevu kama mafuta,tui,maji,n.k
       -tunda linalokaribia kuiva k.m Embe tosa litaliwa kesho
Toza-chukua vitu kama pesa kutoka kwa mtu kuwa ni ushuru, kodi au fidia.
Nadhari -akili nzuri.Pia busara k.m mtu aso nadhari,ng’ombe
Nathari-maandishi ya kawaida kama Insha, hadithi, tamthiliya,riwaya,n.k
Kibofu -fuko la mkojo lililoko tumboni
Kipofu -mtu asiyeona
Kibovu -kisichofaa au kilichoharibika k.m kiti hiki ni kibovu
Kobe –jina la dharau kwa mtu anayeshindwa kufunga katika mwezi wa Ramadhani.
         -mnyama kama kasa mwenye magamba magumu,shingo fupi na aendaye polepole.Pia Furukombe.
Kope -nywele zilizo katika kikawa cha jicho
         -ngozi zinazofunika macho wakati yakiwa yamefumbwa.
         -ncha ya utambi wa taa iliyowashwa.
Chusa -chombo mfano wa mkuki wenye meno matatu cha Kuwavulia samaki wakubwa kama papa, Chewa au
           nguru.
Chusha -kosa kuridhisha.Pia chukiza.
Pora-nyanganya kwa kutumia nguvu.Pokonya au bwakura.
       -jogoo ambaye hajaanza kuwika.
Bora-kitu cha kufaa zaidi au chenye thamani. Pia afadhali.K.m Gari lako ni bora kuliko langu.
Shari-jambo linaloleta hasara au matokeo mabaya.
       -jambo la kumwudhi mtu.Pia ugomvi au chokochoko
Shali-kitambaa cha sufu cha kuvaa begani na shehe.
Zindika -fanya kitu kuwa imara kwa kukifanyia dawa zenye kukinga madhara.K.m Kiwanja hicho
              kimezindikwa dhidi ya wanyakuzi
Sindika -funga mlango au dirisha bila ya kutia komeo wala kubana. Pia Shindika.k.m  Tafadhali zindika mlango ili mdogo wako aweze kuufungua.
Baba – Mzazi wa kiume.
Papa – Aina ya samaki.
Sahibu – Mwandani au rafiki.
Shahibu – Mwanamume mzee.
Dhibiti -Weka sawasawa.
Thibiti – Kuwa ya kweli au ya  kuaminika.
Bibi – Mke wa mtu au nyanya.
Pipi – Aina ya peremende.
Sana– Iliyozidi kawaida.
Sanaa – Ufundi wa kuwasilisha hisia na mawazo ya kibinadamu.
Kula –Tia chakula kinywani na kukimeza.
Kura – Uchaguzi unaofanywa ili kumchagua mtu.
Samani-Vyombo vilivyotengenezwa kwa mbao
Zamani – Kitambo au miaka mingi iliyopita.
Choka – Pungukiwa na nguvu mwilini baada ya kufanya kazi.
Shoka – Kifaa cha kuchanjia kuni.
Kalamu – Kifga cha kuandikia.
Karamu –Vyakula vilivyoandaliwa watu wengi kwa ajili ya shughuli maalum.
Kua – Kuongezeka kwa umri na kimo.
Kuwa – Tendeka.

Komaa – Kuwa mtu mzima.
Koma – Fikia mwisho au hatima.
Bunda –Fungu la vitu kama karatasi au nguo
Punda – Mnyama afananaye na farasi atumikaye kubebea mizigo.
Mahari –- Malipo ya kuolewa au kuoa
Mahali – Masikani au sehemu ya mazingira.
Songa – Kusanya pamoja na kuelekeza upande mmoja.
Zonga – Zunguka kwa mambo mengi.
Sama – Sakama kooni.
Zama – Didimia majini; kale.
Bahasa – Bei ndogo isiyo ghali.
Bahasha – Karatasi iliyokunjwa inayotiwa barua.
Hanja – Zunguka huko na huko kwa majivuno
Haja – Matlaba au mahitaji.
Fuka – Toka moshi.
Vuka – Pita au enda upande wa pili.
Lia- Tokwa na machozi pamoja na sauti hasa mtu akifikwa na huzuni au maumivu.
Ria – Hali ya kufanya jambo kwa ajili ya kutaka kusifiwa.
Fara – Ukingo wa juu wa chombo cha mjazo.
Fala – Mtu aliyepumbaa
Posa – Peleka maombi ya kutaka kuoa kwa mzazi wa mwanamke.
Poza – Malipo apewayo mtu ili kumtuliza kwa jambo.
Ungua-Teketea kwa moto.
Ugua- Patwa na ugonjwa.
Fuja-Tumia mali vibaya.
Vuja– Hali ya kitu kiowevu kama vile maji kupita kwenye sehemu ndogo kama tundu.
Pima- Kukadiria ukubwa, wingi, hali au uzito wa kitu.
Bima- Mpango wa kulipa fedha katika kampuni au shirika ili kupata fidia baada ya muda fulani.

Bata– Ndege afugwaye nyumbani.
Pata – Kuwa na kitu ulichokitarajia.

Vua -Toa nguo mwilini au toa samaki majini.
Fua – Osha nguo. Tengeneza kitu kutokana na chuma.
Msasi – Mtu anayewinda wanyamapori.
Mzazi – Baba au mama.
Mchuuzi-Mtu anayeuza vitu rejareja.
Mchuzi – Kitoweo kiliwacho majimaji.
Doa – Alama juu ya kitu au kasoro.
Ndoa – Harusi au nikahi.
Picha – Umbo la kitu au mtu lililoandikwa, kuchorwa au kupigwa chapa
Pisha– Kumpa mtu nafasi ili apite
Vuta-sukuma kuja upande wako
Futa-Pangusa ondoa uchafu
Randa-Zurura
          -Kifaa cha seremala
Landa-fanana k.m Anamlanda mamaye

Nchi-taifa,Jamhuri
Inchi-Kipimo cha urefu katika rula au mita

mchi-Mti wa kutwangia katika kinu
Mji-Mkusanyiko wa nyumba nyingi,maskani ya watu
     – sehemu ya tumbo la uzazi kwa wanawake ,tumbo la uzazi

Masaibu-Matatizo yanayomkumba mtu
Mashaibu-wanaume wazee
masahibu-marafiki

Jabari-mwenye nguvu
Jabali-jiwe kubwa;mwamba

Fahari-utukufu au majivuno
Fahali-ng’ombe dume

Faa-kuwa na faida
Vaa-kutia nguo mwilini

Daawa-madai au jambo linalosababisha ugomvi
Dawa-Kemikali inayotibu maradhi au kitu anachopewa ili awe katika afya au mienendo mizuri

Asi-goma,kataa kufuata sheria
Hasi-Kumfanya ng’ombe dume kuwa maksai,ondoa makende kutoka kwa mnyama dume

Ama- au,pengine
Hama-hajiri
          -toka katika makao fulani na kwenda kwingine

ngoma – ala ya muziki itoayo sauti inapopigwa
goma –acha kufanya kazi

shindano – makabiliano baina ya watu wawili au zaidi ili kutambua atakayeongoza
sindano –kifaa kinachotumika kushonea vitu

Haba –kisichokuwa kingi
Hapa –mahali karibu

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *