Mwanamke
- Alikuwa mwanamke wa elfu. Hakika, Mungu alikuwa amempoteza hurulaini wake peponi.
- Meno ya bisi/mchele yaliyopangwa yakapangika kinywani kama lulu katika chaza/bao katika vidu/kete.
- Mwanya wa haiba na mvuto /mwanya wa mwangaji.
- Midomo ya miteko na kasiba.
- Vidu vilivyoshobweka barabara mashavuni.
- Urembo wa sahani.
- Macho ya chawa kama Mchina au Maninga ya gololi/kikombe
- Pua ya mtepeto kama Mhabeshi au pua ya kitara.
- Shingo ya upanga
- Masikio ya mchanuko
- Mikono ya mbinu
- Kope zake zilichanwa zikachanika kwa uzuri wa kupendeza na kutamanika.
- Kiuno chake kilichezacheza kwa migwayo ya kumezea na kutamanika.
- Mabega ya mfumbati
- Nywele za julfa zilizofungwa kwa mafundo ya kupendeza na kutaanisi.
- Kiuno cha bunzi au kiuno cha nyigu.
- Miguu ya cherehani bila matege wala mang’ombo/ matege wala maguta
- Alikuwa mfua uji mwenye umbo la shani.
- Aliumbwa akaumbika ungalifikiri Dayani alichukua siku ayami kumwumba.
- Mwingi wa tabasamu.
- Uso wa haiba au uso wa kifuu cha nazi au wajihi wagivu/uso wa nuru.
- Nyusi za mwezi mwandamo/mwezi kongo.
- Kifuani dodo zake (viduta vyake) hazikuachwa nyuma zilisimama imara kama vitumbua viwili vililvyochongwa na mfinyanzi stadi/gwiji/galacha na kutiwa hamira.
- Umbo la wastani
- Kiuno chake kilikuwa sawa na namna yai lilivyo katikati.
- Uzuri wake usingeelezwa kwa maneno matupu.