ULEMAVU

ULEMAVU

walemavu,kenya,ayo tv,nelly wanjiku,autism,uganda,unnews,deutsche welle,unitednations,connie kariuki,habarizaun,millard ayo,mkuu wa wilay,same,k24tv,rwanda,swahili,tanzania,kiswahili,dw




Kilema/Uatilifu –ni kasoro iliyoko kwenye kiungo au viungo vya
mwili.
Mlemavu – ni mtu au mnyama mwenye kasoro ya kiungo au viungo.

A)Hali ya ulemavu

  1. Mafungamavi -Miguu iliyopindika kwa ndani.
  2. Kidazi -Ukosefu wa nywele kichwani.Pia upara.
  3. Kigutu -Kiungo cha mwili kilichokatika.
  4. Upara-Hali ya kutokuwa na nywele kichwani.
  5. Mangombo -Miguu iliyobinukia mbele.
  6. Matege -Miguu iliyopindika kwa nje na kuacha nafasi kati ya mguu mmoja na mwingine.Pia gobwe au magombi 
  7. Magutao -Miguu iliyobinukia nyuma.
  8. Pacha-Kwenda kama mwenye kilema cha miguu.Pia Chechemea au dengua.
  9. Kinyonyoke -Mtu asiyemea nywele kichwani na zikimea hukatika.
  10. Kinyenyezi -hali ya kutoona vizuri.

B)Walemavu mbalimbali


  1. Kipofu -Mtu asiyeweza kuona kabisa.
  2. Chongo -Mtu aliye na jicho moja lililoharibika.
  3. Njorinjori -mtu mwenye miguu mirefu kupita kiasi.
  4. Kiguu-mtu ambaye mguu wake mmoja una kilema aghalabu kupindika.Pia kiguru.
  5. Kibyongo-mtu mwenye nundu mgongoni.Pia kigongo, kiduva au kijongo.
  6. Kisaka -mtu mwenye kimo kifupi.Pia kibirikizi au kidurango.
  7. Chakaramu -mtu aliye na kichaa.Pia afkani.
  8. Chotara -mtu aliyezaliwa na wazazi wa rangi tofauti au mbalimbali.Pia shombe au suriama.
  9. Mziavu-mtu aliyevia akili.
  10. Buge -mtu aliyekatika kidole au asiye na kidole cha mkono
  11. Kikono -mtu mwenye kilema cha mkono.
  12. Mpapachi -mtu aliye na meno yaliyopandana.
  13. Toinyo -mtu aliyekatika pua.
  14. Kigutu –kiungo cha mwili kilichokatika.
  15. Kipara-Mtu asiye na nywele kichwani.
  16. Makengeza -mtu aliye na mboni zisizo katikati bali upandeupande. Pia mawenge.
  17. Mbedu -chongo aliye kengeza.
  18. Bubu -mtu asiyeweza kusema kabisa.
  19. Kigugumizi-nmtu anayesita katika kusema au kusoma Pia kitata.
  20. Kithembe -mtu anayetamka aneno kivyake kwa ncha ya ulimi,
  21. Kiziwi-mtu asiyeweza kusikia.Pia kiduko,
  22. Masito –mtu asiyesikia vizuri lakini si kiziwi.
  23. Kibwiko -mtu mwenye vidole vilemavu.
  24. Kigego -mtu anayezaliwa akiwa tayari na meno au mtoto ambaye meno ya juu yametangulia ya chini
  25. Kibogoyo-mtu asiye na meno au mwenye meno machache. Pia mhangi.
  26. Kibunye-mtu aliyekatika sikio au masikio yote.
  27. Kiwete -mtu aliyelemaa miguu yote.
  28. Buda-mwanamume mzee sana aghalabu asiye na meno.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *